Friday, February 29, 2008

"Daraja la Mungu"

Tanzania ina mambo mengi ya kuvutia na ya ajabu. Ukibahitika kusafiri kwenda mkoa wa Mbeya wilaya ya Rungwe karibu na Chuo cha Magereza cha Kiwira. Mto wa Kiwira unapita chini ya mwamba mkubwa na kufanya kuwa daraja. Daraja hilo ni kubwa na linajulikana kwa jina la “Daraja la Mungu.” Nilibahatika kuliona daraja hilo mwezi wa Desemba, 2008. Sehemu hiyo ikitengenezwa vizuri ni moja ya vivutio vya watalii mkoani Mbeya na nchini. Moja ya chanzo cha mapato kupitia sekta ya Utalii. Tuchanganke!

No comments: