Tuesday, February 12, 2008

MABUS YA VICTORY NI MFANO MBAGALA

Nimekuwa nikisafiri kuelekea Mbagala mara kwa mara kwa kutumia daladala.

Mbagala kuna wakazi wengi sana. Mbagala kuna daladala nyingi sana. Kwa kweli njia ya Mbagala haikauki abiria. Kwa muda wote huo nimekuwa nikuchunguza jinsi daladala zinavyotoa huduma kwa abiria wa Mbagala.



Mabus ya VICTORY yamekuwa yakitoa huduma bora na ni mfano wa kuigwa. Kwanza mabus yake yako katika hali nzuri, pili ndani kuna burudani safi inayomfanya abiria asichoke na safari, tatu huiwabugudhi wanafunzi, nne haikai hazipotezi muda bila sababu kwenye vituo, tano hayana tabia ya kujaza mafuta kwenye vituo vya mafuta wakiwa na abiria, sita nadra kukatisha njia, saba dereva na kondakta daima ni wasafi na wako katika sare zao, nane hazikamatwi hovyo hovyo na traffic, tisa hawalazi damu katika kurudisha chenji, kumi wahudumu wana lugha nzuri kwa abiria.

No comments: