Friday, February 1, 2008

MADEREVA AKINA MAMA WAKO MAKINI

Kwa muda mrefu nimekuwa nikichunguza uendeshaji wa magari kwa akina mama. Nimegundua kuwa akina mama wengi madereva wako makini sana kwenye uendeshaji kuliko akina baba.

Hebu chunguza ajali nyingi za barabarani zinazotokea hapa Dar. Zilizo nyingi wahusika ni akina baba.

Mwanamke akifahamu kuendesha gari kwanza anazingatia sheria za uendeshaji halafu anajijali yeye mwenyewe pamoja na abiria wake. Lakini wanaume wengi wanajifanya wao wanajua sana kuendesha. Watayapita magari kwenye mlima, kwenye kona na pengine kusiko ruhusiwa. Matokeo yake ni ajali zisizo na msingi. Halafu tunasema bahati mbaya! Ajali zinaua na kutesa pengine kuliko ukimwi. Tuwe waangalifu wanaume madereva.

Hongera akina mama na dada zetu kwa uendeshaji makini!

No comments: