Friday, February 1, 2008

DALADALA HILI MBAGALA R3/BUGURUNI

Daladala T848 ASY-S.1887G. Lenye njia ya Mbagala R3 - Buguruni kwenye kioo cha mbele cha gari yameandikwa maneno " No Discation." kwenye tikiti za bus hilo pia imeandikwa "No Discation." Nimeshindwa kupata ujumbe wa maneno hayo. Nimeangalia kwenye kamusi ya Kiingereza nimeshindwa kupata maana ya neno "discation."

Huenda alitaka kuandika " No Discussion" kwa kiswahili chepesi yaani hakuna mazungumzo, majadiliano au "POA" lakini jinsi lilivyoandikwa kwenye bus lile halina maana kabisa.

Kweli tunapenda kutumia maneno ya kiingereza ili "kuweka msisitizo" wanasema watoto wa mjini, lakini basi tuandike kiingereza sahihi vinginevyo hutueleweki kama nilivyoshindwa kupata ujumbe ulioandikwa kwenye bus hilo.

Si kwenye magari tu. Lakini tumekuwa tukikosea maandishi ya kiingereza kwenye sehemu nyingi tu k.m. "Gerege!" badala ya Garage.

Tuwe makini katika kutumia lugha mbalimbali. Na kama hatuzifahamu vizuri basi tuache kuzitumia au tuwaulize wenzetu wanaozifahamu.
Hivi kwanini tusiandike kwa kiswahili au hata kwa lugha zetu za asili/kabila?

No comments: