Friday, February 1, 2008

Mkuranga:-Mtajikomboa kwa kilimo cha mboga na matunda

Wilaya ya Mkuranga ni moja ya wilaya za mkoa wa Pwani.

Kiuchumi wilaya hii hutegemea sana zao la korosho na nazi kwa kiasi kidogo.

Lakini miaka ya hivi karibuni baada ya kukamilika kwa barabara ya Kilwa ipitayo katika wilaya ya Mkuranga. Maisha ya jamii yamebadilika sana. Watu wa Pwani si wavivu tena. Wapwani wameanza kujishughulisha na kilimo cha mboga mboga na matunda. Wilaya ya Mkuranga kwa sasa inazalisha matikiti maji mengi na mazuri karibu kwa wakati wote. Mkuranga sasa inazalisha mbogamboga nyingi hasa mchicha, Mkuranga matunda ya "passion". Ikizingatiwa kuwa upatikanaji wa maji ya visima ni mkubwa katika vitongoji vya Mkuranga umwagiliaji hutumika ingawa kwa vifaa duni. Wakulima wanafahamu sasa kuwa kilimo kinalipa. Hebu tembelea Kisemvule stendi uone jinsi biashara ya smadi ya kuku ilivyoshamiri, wakulima hutoka sehemu mbalimbali kununua samadi ya kuku. Nayo biashara hii ya mbolea inalipa!

Wakulima wameanza kubadili maisha yao. Wengi wameanza kujenga nyumba za kisasa, wengi wamenunua baiskeli na sasa watoto wao wanapata elimu ya Sekondari kwenye shule ya Sekondari Vikindu. Hayo ni maendeleo. Vitu kama hivi havikuonekana miaka mitano iliyopita. Leo mtu anaona fahari kuitwa mkulima kwa kuwa kilimo kinalipa.

2 comments:

Unknown said...

Nauliza ninashamba heka2 mkuranga nataka kulima passion

Unknown said...

Jee liko wapi soko lake?