Friday, February 29, 2008

Mwanafunzi anapokuwa mwizi

Hivi karibuni kuna matokeo mawili yaliyotokea yanayofanana lakini yamefanyika katika sehemu mbalimbali. Moja limetangazwa kwenye vyombo vya habari lakini moja bado halijatangazwa. Matokeo yote mawili ni ya wizi. Matokeo yote mawili wahusika ni wanafunzi. Moja linamuhusu mwanafunzi wa shule ya sekondari na mwingine shule ya msingi. Moja limetokea mkoani Pwani lingine Mkoani Mbeya. Mmoja ameuwawa kama jambazi aliyekutwa na silaha akitaka kuiba kwenye shule anayosoma mwenyewe. Mmoja amekutwa akiiba dawati kwenye shule ya msingi Kisemvule mkoani Pwani.

Matukio yote mawili si ya ajabu lakini ni ya kushangaza. Wezi wanafunzi. Wezi wanaibia shule zao wenyewe. Hawa bado ni vijana wadogo je watakapoanza kazi itakuwaje. Tutafakari.

No comments: