Tuesday, February 12, 2008

SIKU MOJA TUTALIA SANA!

Siku moja Taifa litaomboleza msiba mkubwa tusipokuwa waangalifu.

Wanafunzi wanaosoma katika shule zilizopo kwenye barabara ya Kongowe - Kigamboni wana matatizo makubwa ya usafiri.

Magari ya daladala yaliyopo mengi huwapiga chenga. Matokeo yake wengi husafiri kwa magari ya kubeba mchanga. Iwe mvulana au msichana ni kudandia tu malori. Wengi hufika shuleni wamechafuka na wengine kuumia. Si vibaya sana, lakini ninachoogopa mimi ni kutokea kwa ajali. Magari haya huenda kwa mwendo wa kasi huku wanafunzi wakiwa juu kabisa ya malori.

Sawa wanasaidiwa usafiri lakini iko siku moja tutalia Taifa zima. Naomba hatua za haraka zichukuliwe kunusuru hilo lisije kutokea

No comments: