Friday, February 29, 2008

Kilwa Road Mkeka umeanza

Ndiyo, Kampuni ya Kajima imeanza kuweka “mkeka” (lami) kwenye barabara ya Kilwa ingawa kwa vipande vipande lakini inatia moyo sana. Kajima ilianza kama mchezo lakini barabara ile wameijinga strategically walianza kujenga ‘culverts” madaraja na mifereji. Wakamwaga vifusi. Sasa hawana wasiwasi na masika tena kwani hata kushindilia wameshashindilia. Kilichobaki ni lami na nakshi nakshi. Sasa Mbagala kumekucha! Tatizo la foleni ni historia. MADCM yameanza kupungua kwa kasi ya kufurahisha. Buguruni-Mbagala tunaona “Pamba nyepesi” ya Civilian. Nasikia watakabidhi barabara (Hadi Mtoni Mtongani) mwezi Aprili, 2008. Kazi nzuri sana KAJIMA

No comments: