Friday, February 29, 2008

Wachezaji wanapojisahau kula "Pilau" kablaya mechi!

Juzi pale Kisemvule, kulifanyika pambano la fainali kugombea mbuzi kati ya Timu ya TanBlock (Ksemvule) na Motohaulambwi (Vikindu). Tanblock walikuwa wanauwa ndege wawili kwa jiwe moja. Kwanza walikuwa wanaifungua rasmi kampuni yao ya kufytatua matofali ya TanBlock kwahiyo ilifanyika Maulid kubwa pale. Mchele kilo 150. Pilau ililika saa 8 mchana na mechi kuanza saa 10.30. Inasemekana kuwa karibu wachezaji wote wa Tanblock walikula punga lile. Huku wakiwa na matumaini makubwa ya kumbeba mbuzi (yaani kushinda mechi). Mambo hayakuwa hivyo.

Katika kipindi cha kwanza Motohaulambwi waliandika bao la kwanza na katika kipindi cha pili wakaongeza bao la pili kabla Tanblock hawajasawazisha na hatimaye “Moto” kubeba mbuzi.

Utakulaje “Pilau” chakula chenye mafuta mengi ambayo huchukuwa muda mrefu kuyeyushwa masaa machache kabla ya kuingia uwanjani? Pilau “iliwaloga” Tanblock. Tanblock hawakuwa na mshauri kuhusu mechi ile.

No comments: