Friday, February 29, 2008

Kijungu

Mkoa wa Mbeya una maajabu mengi lakini hayjatangazwa. Moja ya maajabu hayo ni sehemu inayoitwa “KIJUNGU” iliyopo ndani ya mto Kiwira, wilayani Rungwe ndani ya na Chuo cha Magereza Kiwira..Hapa maji yanapita chini ya mwamba kwa kina kirefu sana na yanazunguka. Kuna maelezo mengi yanayotolewa na wenyeji kuhusu sehemu hiyo. Lakini utafiti wa kina haujafanyika. Na kama umeandikwa basi uko kwenye makabrasha kama ilivyo kawaida yetu. Wasomi mpo? Hapa yanaweza kuandikwa mengi katika nyanja mbalimbali. Changamkieni tenda. Mnaweza kupata shahada mbalimbali kutokana na “KIJUNGU”

No comments: