Tuesday, February 12, 2008

NAMIBIA WANAPIGIA DEBE KISWAHILI

Nimekamata gazeti la "Daily News" la Februari 2/2008. Namsoma Kiangiosekazi wa Nyoka kutoka Windhoek.

Barua hii kutoka Namibia pamoja na mambo mengine, Rais wa Namibia Hifikepunye Pohamba anakifagilia sana Kiswahili na anasema hana neno kwa kukiona Kiswahili kuwa lugha ya Afrika. Anasema, jitahada za kutosha hazijafanywa kukifanya Kiswahili kuwa lugha ya Taifa. Anaongeza kuwa, utashi wa kisiasa ya Namibia unakipa nafasi kubwa Kiswahili kuwa lugha ya Afrika.

Kwa hili nani wenye nafasi kubwa? Wanamibia au Watanzania? Tuchangamke.

No comments: