Thursday, August 27, 2009

2nd CHANCE MKOMBOZI WA KISEMVULE

Kama kuna wafanyabiashara wanaoona mbali na kujizatiti kutoa huduma kwa umma basi ni mmiliki wa bus linaloitwa 2nd Chance linalofanyakazi kati ya Mbagala R3 na Kisemvule-Mkuranga.
Bus hili ni zuri na la kisasa, halibagui abiria nikiwa na maana wanafunzi. Wote kwake sawa. Mwanafunzi akikalia seat habuguzwi ni jukumu la mwanafunzi mwenyewe kutambua kuwa ni vizuri kuacha nafasi hizo kwa wazee na isitoshe hulipa nauli ya mwanafunzi.

Kabla ya 2nd chance kuanza kutoa huduma kwenye njia hiyo, wakazi wa Kisemvule walikuwa wakinyanyasika sana na wasafarishaji. Magari yaendayo Mkuranga yalikuwa yakiwaacha wakidai kuwa nauli hailipi. Mengine yalikuwa yakigeuzia Vikindu. Ilikuwa ni karaha kwa wakazi wa Kisemvule.

Ikumbukwe kuwa Kisemvule ni kijiji kinachukua kwa kasi ya kutisha, isitoshe kinafikika kirahisi na kina miundo mbinu imara kama vile umeme na maji ndiyo maana wahamiaji kijijini hapo wanamiminika kwa wingi tofauti na miaka ya 90. Thank you 2ND CHANCE kwa huduma bora

No comments: