Wednesday, August 26, 2009

Shujaa wa Mpango wa Elimu Bure azikwa Kenya


Mwili wa Bw Stephen Kimani Maruge kutoka Kenya umezikwa tarehe 25/8/2009 katika makaburi ya Arashi wilaya ya Nakuru,Kenya akiwa na umri wa miaka 89. Marehemu aliingia kwenye vitabu vya kumbukumbu za maajabu ya dunia (Guiness book) baada ya kujiunga na darasa la kwanza akiwa na umri wa miaka 84.

Bw. Maruge alianza kupata umaarufu mwaka 2003 wakati alipojiunga na darasa la kwanza katika shule ya msingi Kapkenduiywo iliyopo mkoani Eldoret baada ya serikali kutangaza mpango wa kutoa elimu ya msingi bure na haraka akawa kipenzi cha vyombo vya habari.

No comments: