Thursday, August 27, 2009

Dr. Msabaha astaafu baada ya miaka 60


Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo/Mkurugenzi Msaidizi Utafiti wa Mazao katika Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Dr. Mohamed Msabaha amestaafu kuwa mtumishi wa umma tarehe 20/8/2009 baada ya kulitumikia taifa kwa takriban miaka 34.

Katika hafla fupi aliyoandaliwa na watumishi wa Idara yake waliopo makao makuu Dar Es Salaam ilielezwa kuwa Dr. Msabaha alikuwa mtafiti na kiongozi hodari aliyechapa kazi kwa bidii na kwa ufanisi mkubwa katika mazingira mbalimbali.

Baadhi ya mambo aliyofanikisha wakati akiwa kazini ni pamoja na:-
  • Kuanzisha na kuendeleza programu ya utafiti wa mazao ya mizizi hapa nchini (muhogo, viazi vitamu, na viazi mviringo)
  • Moja ya wakurugenzi wakanda waanzilishi wa mfumo wa Utafiti wa Kanda (Zonal Research System)
  • Kiongozi mwanzilishi wa uzalishaji wa mbegu za mazao kwenye vituo vya Utafiti ambao ni endelevu hususan katika kituo cha Utafiti wa Kilimo Uyole
  • Kuongoza kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Uyole kwa mara ya kwanza katika mfumo wa serikali
  • Kusimamia uanzishwaji wa "Regional Rice Centre of Excellency' kitakachokuwa na makao makuu KATRIN-Ifakara.
Dr. Msabaha alianza kazi mwaka 1975 katika kituo cha Utafiti Ukiriguru baadaye alihamishiwa Uyole, Mbeya mwaka 1993 akiwa Mkurugenzi wa Utafiti wa Kanda kabla ya kupelekwa Makao Makuu ya Wizara akiwa Mkurugenzi Masaidizi wa Utafiti wa Mazao mwaka 2007. Mwanzoni mwa mwaka 2009 alikaimu nafasi ya Mkurugenzi wa Idara hadi alipostaafu.

1 comment:

Qasim said...

My uncle by virtue of being a good friend of my uncle's. I was a small boy when he came to Ukiriguru and mmediately became an active member of the local community. With him, Shamte Shomari, Ali Mahmoud, the late Gambishi, EAV Mmari, Ms Bwenge and Mussa Kulembwa the community thrived. I sometimes look to those years and wonder what went wrong for our country's research potentials all of a sudden. Back then, I could overhear them talking of hybrid seeds developed at Ukiriguru. Of course there was an expatriate community too - Dr Lee, Dr Nikolov and others - but the locals were really committed to their cause too. Corruption was unheard of and people at various epartments - pathology, etomology and others dwelt on their tasks. Over thirty years on, my uncle, now retired, laments helplessly in a remote village....