Friday, August 28, 2009

Kila mfanyakazi wa kilimo kuwa na Mpango Kazi -Wasira


Tarehe 9-10 Agosti 2009, Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika ilikuwa na Kikao cha Baraza la Wafanyakazi mjini Dodoma ndani ya Dodoma Hoteli. Kikao hicho kilifunguliwa rasmi na Waziri wa wizara hiyo Mhe. Stephen Wasira.

Agizo moja muhimu alilolitoa ni kuhakikisha kuwa kila mfanyakazi wa wizara anakuwa na mpango wa kazi kwa mwaka 2009/10 ili baadaye apimwe kutokana na malengo aliyojiwekea.

No comments: