Wednesday, April 22, 2015

Harusi ya Bw & Bibi Joachim Ndunguru haikuwa na makuu




Tarehe 11 April, 2015, mimi na mke wangu Mwl. Nancy tulisimamia harusi ya Bw & Bibi Ndunguru tunaoishi nao hapa Kisemvule na kusali kwenye Kanisa la Mt. Vinsenti wa Paulo, Parokia ya Vikindu. Kilichonifurahisha katika harusi hii ni jinsi mipango ilivyoandaliwa na kutekelezwa kwa wakati. Tuliwahi kufika Kanisa, ibada ikafanyika. Mimi na mke wangu tulibahatika kusoma masomo ya siku hiyo. Waumini waliohudhuria walikuwa wachache, lakini kwaya ya Mt. Petro ilitumbuiza kuanzia kanisani hadi nyumbani. Hakukuwahi kufanyika hata kikao kimoja cha maandalizi. Lakini waliokaribishwa walipata chakula na vinywaji na usafiri kutoka kanisani ulikuwepo. Mimi nikiwa 'Best Man' katika harusi hiyo nilipata fursa ya kufungua champaigne na kuwagawia wageni waalikwa. Wanajumuiya ya Mt. Joseph Mfanyakazi ni moja ya kikundi kilichofanikisha harusi hii ambapo shughuli za kuwapokea maharusi zilifanyika nyumbani kwao Kisemvule. IDUMU NDOA HII. MILELE AMINA.

No comments: