Wednesday, May 13, 2015

St. Francis Secondary School ya Mbeya yakabidhiwa Tuzo

Wengi tunaisikia St. Francis Secondary School  ya Mbeya. Ni shule inayofanya vizuri kitaaluma. Imekuwa ikishikilia nafasi 10 za juu za ufaulu hapa nchini karibu kila mwaka. Shule hii iko makini sana katika kudahiri wanafunzi wanaojiunga na shule hiyo. Si rahisi kupata nafasi kama kijana hana uwezo. Na anapojiunga na shule hiyo pamoja na ukweli kuwa iko vizuri kitaaluma lakini wanaangalia sana nidhamu ya mwanafunzi.Wanafunzi wanatakiwa kuchapa kazi wakiwa shuleni, kutambua kuwa MUNGU yupo na kumwabudu. Nimeambiwa kuwa hakuna kujidai ukiwa shuleni hapo kama baba au mama yako ni Waziri, Mbunge,Mkurugenzi, Profesa au Meneja hiyo ni kwenu. Hakuna kuleta majidai ukiwa shuleni hapo. Pichani Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda akikabidhi Tuzo kwa mwakilishi wa shule hiyo mjini Dodoma hivi karibuni.

No comments: