Wednesday, May 13, 2015

Teknolijia zinavyosambazwa na Taasisi zinavyojitangaza India





Mwaka jana nilibahatika kuwa katika msafara wa mafunzo nchini India. Madhumuni ya msafara huo ni kujifunza jinsi wenzetu wa India wanavyoendesha Taasisi za Utafiti. Moja ya kitu ambacho nimevutiwa nacho ni jinsi wanavyotunza kumbukumbu na jinsi wanavyosambaza teknolojia za kilimo na jinsi taasisi zinavyojitangaza. Kikubwa wenzetu ni wazalendo. Hata katika lugha, mabango yote yanatanguliwa na lugha yao na kufuata Kiingereza hii haidhoofishi sayansi, badala yake inakuza sayansi kwani mtu anafanya kitu anachokielewa na pia wadau wanafaida nacho.

Unapopokelewa katika taasisi kabla ya kupata maelezo ya shughuli za kituo hicho, unawekewa clip yenye nyimbo ya Taasisi na wote wanajivunia. Nyimbo inapoimbwa unajionea na kusoma historia ya taasisi, shughuli wanazofanya na mafanikio waliyoyapata. Na hiki ndicho tumekishauri kwa Taasisi zetu za Utafiti kuiga, kwani gharama yake si kubwa kama inavyodhaniwa. Angalia mabango hayo hapo juu yanajitosheleza. Kwa njia hii teknolojia inasambazwa kwa haraka na Taasisi inajitangaza.

No comments: