Thursday, September 3, 2009

BABA WATAIFA ALISEMA NINI KUHUSU KILIMO?

Kwa sababu ya umhimu wa kilimo katika maendeleo yetu ingetegemewa kuwa kilimo na mahitaji ya wakulima yangekuwa ndio chanzo cha kupewa kipaumbele katika utayarishaji wa mipango yote ya uchumi wetu. Badala yeke tumechukulia kilimo kama sekta ya pembezoni au kama shughuli nyingine yoyote ya kawaida ambayo inatumiwa na sekta nyingine bila yenyewe kupewa umuhimu wowote ule.... Tunakipuuza kilimo; kama tungekuwa hatukipuuzi, basi Wizara zote, mashirika ya umma yote na mikutano yote ya chama ingekuwa inafanya kazi kushughulikia mahitaji ya wakulima. Ni lazima sasa tuache kukipuuza kilimo. Ni lazima tukifanye kilimo ndio shina na mwanzo wa mipango yetu yote ya maendeleo. Kwani kwa hakika, kilimo ndio msingi wa maendeleo yetu.

Baba wa Taifa, Mwalimu Julius K.Nyerere-1982

No comments: