Friday, September 4, 2009

Ikiwa hatutambui umuhimu wa choo kwa wanafunzi wetu kazi kwelikweli


Shule ya Msingi Mnyamasi (Sijui iko wilaya na mkoa gani). Wanafunzi wa shule hiyo wanaonekana pichani wakipishana kwenda chooni. Angalia choo chenyewe. Hivi tunangojea akina nani watujengee vyoo. Wazazi, walimu hata viongozi wa kijiji hicho, kata na wilaya kweli hatutambui umuhimu wa kuwa na choo bora katika shule zetu? Tunangojea JICA watujengee choo kweli katika karne hii? Picha hii inaonekana katika Majira ya leo tarehe 4 Septemba 2009 uk.1

No comments: