Friday, September 4, 2009

Tunapozika 'mgomba'


Mara nyingi nimewahi kusoma au kusikia kuwa ah "wale wamezika tofauti zao" ikiwa na maana wamekubaliana kitu fulani ambacho hapo awali walikuwa na mawazo tofauti. Hapa nchini mambo haya yametokea mara nyingi kwenye vyama vya siasa. Hivi karibuni chama cha CHADEMA kiliingiwa na mtafuruku fulani kwa viongozi wenye mvuto ZITTO KABWE na FREEMAN MBOWE wote kuwania nafasi ya UENYEKITI kwenye chama hicho. Lakini baada ya ushauri wa ndani na nje ya chama hicho inasemekana kuwa wote wawili wamezika tofauti zao na sasa wote lengo lao ni kukijenga CHADEMA hasa wakati huu wanapoelekea kwenye uchaguzi wa Kitaifa wa mwaka 2010. Ndiyo maana Mchora kikatuni Nathan anataka kujua kweli wamemaliza tofauti zao au wamezika "mgomba?" Picha kwa hisani ya gazeti la Majira 4 Septemba 2009.

No comments: