Friday, September 4, 2009

Jamani Mwakyembe!


Gazeti la Majira la leo tarehe 4 Septemba 2009 uk. 4 limeandika habari ya Mwakyembe kunususrika kuchomwa kisu tena nyumbani kwao Kyela wakati akihutubia mkutano wa hadhara. Kwa mujibu wa gazeti hilo, Dkt. Mwakyembe amekiri kutokea tukio hilo alipohojiwa kwa njia ya simu.Inasemekana kuwa walinzi wake Dkt. Mwakyembe waligundua mapema njama hizo na walipojaribu kumkaribia mmoja wa vijana waliohisiwa alikimbia na kudondosha kisu na mwingine wa pili alipokamawatwa alikutwa na simu aina ya Sonny Erricson na vinasa sauti.

Mei 21 mwaka huu Dkt. Mwakyembe alipata ajali ya gari huku kukiwa na taarifa tata zinazopingana, moja ikiweka wazi kwamba gari lake liligongwa na lori ambalo halikukamatwa mara moja na nyingine ikidai kwamba dereva wake aligonga shimo na kukosa uelekeo linaandika gazeti hilo la kila siku hapa nchini.

No comments: