Friday, September 18, 2009

LULU anahamasisha TUGHE


Si jambo la kawaida kwa mzazi kumshirikisha mtoto wake kwenye shughuli za kitaifa tena ikiwa mtoto mwenyewe ni binti. Si hivyo kwa Bw. Omari Shomari mfanyakazi wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika aliyekuwa tayari kwenda kwenye maandamano ya Sherehe za Wafanyakazi mwaka huu zilizofanyika mkoa wa Dar ES Salaam kwenye uwanja wa UHURU. Pichani Bi Lulu Shomari akifurahia maandamano akiwa na baba yake Omari Shomari, Banzi wa Moro na Salehe Mkwawa (Mzee wa Yanga) tarehe 1/5/2009. Bw. Omari Shomari ni mwanachama mwanzilishi wa TUGHE-KILIMO MAKAO MAKUU. Kweli Lulu anahamasisha TUGHE.

No comments: