Wednesday, September 30, 2009

Afadhali kuwa na pikipiki

Mwishoni mwa juma la jana nilisafiri kwenda kijijini Matombo. Kipya nilichoona ni usafiri wa pikipiki ulivyopamba moto. Nilikuta pikipiki Kiroka, Mkuyuni, Njia panda ya Kinole na Mtamba. Hii ina ashiria nini? Usafiri vijijini unaanza kuboreka. Baiskeli zinaanza kupungua kidogo kidogo. Hii ni hatua kubwa ya maendeleo. Tulitembea kwa miguu, baadaye wachache wakabahatika kuwa na baiskeli lakini tulianza kurukia magari kabla ya kuwa na pikipiki. Tumerudi mahali pake ndo maana nasema afadhali kuwa na pikipiki kuliko kutembea kwa miguu. Lakini pikipiki hizi zitumiwe kwa uangalifu la sivyo zitaleta madhara kwa jamii.

No comments: