Thursday, October 1, 2009

Komunio ya Kwanza -Matombo


Sikukuu ya kupata Komunio ya Kwanza kwa waluguru wa Matombo ni Sikukuu kubwa isiyofanyiwa mzaha hata kidogo. Maandalizi kwa watoto ya kiroho na kimwili ni makubwa na sherehe ni nzito. Banzi wa Moro alishuhudia sherehe kabambe za Ekaristi katika Kanisa la Watakatifu Petro na Paul Matombo. Ibada iliyoendeshwa tarehe 27/9/2009 katika Parokia hiyo ni ya kukumbuka. Siku hiyo pia kinanda kipya kilichonuliwa na waumini pamoja na wafadhili wazalendo kilichezwa kanisani. Pichani watoto waliopata ekaristi wakibebwa kuelekea nyumbani huku ngoma ikiwasindikiza - Nafikiri ilikuwa sh2!

No comments: