Friday, October 2, 2009

Huyu ndiye Dkt Alfred Moshi wa mahindi


Wadau wa Kilimo hapa nchini hasa wa kanda ya Mashariki unapozungumzia mahindi basi akilini mwao unamzungumzia Dkt. Alfred Moshi aliyekuwa Mkurugenzi wa Utafiti Kanda ya Mashariki. Moshi kwa muda mwingi amekuwa akitafiti mbegu bora ya zao la mahindi. Pichani Dkt Moshi akitoa neno kwa niaba ya watafiti waliostaafu mwaka 2008/09 kwenye viwanja vya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika - Kilimo II kwenye tafrija ya kuwaaga waliyoandaliwa na Idara ya Utafiti na Maendeleo tarehe 3/07/2009

No comments: