Saturday, October 24, 2009

Hawakujiandikisha kwasababu mambo ni yaleyale


Uchaguzi wa viongozi wa Serikali za mtaa na vijiji unatarajiwa kufanyika kesho. Wananchi wengi inasemekana kuwa hawakujiandikisha. Ni kweli, Banzi wa Moro katika pitapita yake mjini na vijijini amegundua kuwa watu wamekata tamaa na uongozi wa vijiji na mitaa kwani kasi ya maendeleo hasa huko vijijini ni kidogo sana. Mambo ni yale yale. Viongozi wanaomba nafasi hizo kwa manufaa yao binafsi na wala si ya wananchi. Utasikia ah nikipata nafasi hii baada ya muda wangu wa uongozi kumalizika lazima ninunue 'daladala.'Hivi ndiyo lengo kweli la kugombania uongozi ? Wakati wa kampeni nimeshuhudia vibweka vingi kwa vyama vyote wakishindana kwa rusha roho! Hivi kweli kuna lolote hapa? Ndo maana wengi hawajajiandikisha! (Picha kwa hisani ya gazeti la mwananchi tarehe 24 Oktoba 2009)

No comments: