Friday, July 1, 2011

Mkude wa Morogoro


Huyu ni ndugu 'mtoto' wangu anaitwa Mkude. Kwa kuzingatia taratibu za mila za Kiluguru mimi ni Baba Mkude. Lakini mimi ni Banzi au Jaka, Zinga na dada zangu wanaitwa akina Kimbiki ni watoto wa Wambiki. Watoto wangu wanastahili kuitwa akina Mkude, Mizambwa, Mdoti, Midahuli.. (wanaume) na ikiwa mwanamke anaitwa Mwenda au Mlamwenda. Kwa hiyo huyo ni ndugu yangu na ni mtoto wangu. Morogoro akina Mkude,Banzi, Mloka, Mwenda, Mbiki,Mbena, Luanda, Mtonga tukiwa nyumbani tunatumia jina la kwanza kutotofautisha!

No comments: