Friday, April 23, 2010

He kumbe aghali hivyo?


"Kuwekeza kwenye ICU siyo kitu rahisi.Gharama yake ni takribani sh 250 milioni kwa kitanda kimoja chenye huduma zote hizo." Maneno haya yalisemwa na Dk. Mpoki Ulisubisya. Dk.Mpoki aliyasema hayo kwenye maonyesho ya kuadhimisha miaka 10 ya lilokuwa Shrika la Afya Muhimbili ambalo sasa ni Hospitali ya Taifa ya Muhimbili yaliyofanyika wiki lililopita. Magonjwa yanayoongoza hapa nchini kwa kuwa na wagonjwa wanaolazimika kufikishwa ICU ni wale wenye matatizo ya kuwa na usaha tumboni, kifafa cha mimba, pepo punda, kiharusi, wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wa moyo, walioumia kichwani, majeruhi wa ajali, figo, kisukari na watoto wenye shida katika njia ya hewa. ICU ni kifupi cha 'Intensive Care Unit' kwa kiingereza. Kweli ICU ni aghali lakini ni muhimu kwa maisha yetu.

No comments: