Saturday, April 3, 2010

Ali Hassan Mwinyi na Azimio la Arusha


Rais wa awamu ya pili Mhe. Ali Hassan Mwinyi amesema kuwa, kufilisika kwa mashirika zaidi ya 400 ya umma nchini kulitokana na waliokabidhiwa dhamana ya kuyaongoza pamoja na Watanzania kwa ujumla kutojua maana sahihi ya ujamaa. "Wengi wanadhani kuwa Azimio la Arusha limefutwa na wengine wanadai kuwa Azimio la Zanzibar ndilo lililofuta Azimio la ARUSHA, lakini ukweli ni kwamba Azimio la Arusha halijafa." Mwinyi aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Benki ya Mkombozi ya Kanisa Katoliki nchini iliyofanuyika jijini Dar Es Salaam tarehe 18 Machi 2010.

No comments: