Monday, April 2, 2012

Inawezekana

Essau Banda (katikati) ni Mhasibu - Benki Kuu Malawi na pia ni Mchungaji(Pastor).Tupo naye Swaziland hapa chuoni Mananga. Juzi tulisafiri naye kwenda Maputo Msumbiji. Kabla ya kuanza safari yetu tuliomba mmoja wetu aombe kwa sala ili Mungu aibariki safari yetu. Banda alijitokeza na kuomba sala fupi na nzuri.Kwenye bus nilikaa karibu naye pembeni yake kulikuwa na kitabu. Nilimuomba kukisoma ndipo nipogundua kuwa Banda ni mchungaji baada ya kusoma ukurasa wa kwanza ulioandikwa Pastor Essau Banda! Ona, Banda hajawahi kujionyesha kuwa ni mchungaji au mlokole. Na pia sikutegemea kuwa na mchungaji akisoma mambo ya dunia hapa Mananga, kumbe yote inawezekana!

No comments: