Wednesday, May 30, 2012

Skimu ya umwagiliaji kijiji cha Mkungugu

Ujenzi wa Bwawa la Mkungugu, lilipo katika kijiji cha Mkungugu wilaya ya Iringa Vijijini lilianza kujengwa msimu wa mwaka 2009/10 chini ya Progamu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo (ASDP) lengo ni kukusanya maji ya mvua kwa lengo la kuendesha kilimo cha umwagiliaji.Litakapokamilika, bwawa hili litakuwa na uwezo wa kumwagilia hekta zipatazo 80.Mazao yanayatarajiwa kumwagiliwa ni yale ya bustani pamoja na mahindi. Banzi wa Moro imeshuhudia sehemu kubwa ya bwawa hilo likiwa limekamilika isipokuwa miundo muhimu ya umwagiliaji haijatengmeaa kama vile matanki, pump na mifereji ya umwagiliaji.

No comments: