Monday, June 8, 2015

Maonesho ya Carmel Pre & Primary School-Vikindu 2015









 Juzi Jumamosi tarehe 6/6/2015 nilihudhuria maonesho ya sayansi ya 'Carmel Convent Pre & Primary School' iliyoko Vikindu, wilaya ya Mkuranga, mkoa wa Pwani. Shule hii inaendeshwa na Masista wa Kanisa Katoliki wa Shirika la Mlima wa Carmel. Wanafunzi wakishirikiana na walimu wao waliandaa maonesho hayo. Watoto wenye vipaji waliochaguliwa walionesha uwezo na umakini mkubwa katika kuelezea vitu walivyoviandaa na pia kutuuliza maswali. Hongera sana walimu na wanafunzi.Mimi ni mmoja wa wazazi waliojifunza na kujikumbusha mengi katika maonesho hayo.













No comments: