Friday, December 1, 2006

NAJARIBU KUWA MWANA BLOG


Watanzania wenzangu na wote wanaofahamu lugha ya Kiswahili.

Nabisha hodi.

Ni hivi karibuni tu ndipo nimepata kuelewa blog ni nini. Nilikuwa nasikia blog blog! Lakini baada ya kusoma na kuona mambo mbalimbali kupitia blog mbalimbali. Nimeaona kwanini nisiingine kwenye mtandao wa wanablog? Bado mchanga katika teknolojia hii, lakini nimeipenda. Kwanza kabisa mimi napenda kutoa habari hasa kwa njia ya maandishi. Napenda watu wafahamu ninayoyafahamu mimi, niliyoona mimi na kuyajua mimi. Naomba mnielekeze. Asante Ndesanjo, asante Mjengwa, asante Michuzi, Jeff, Makene, Msaki, Mongi, Dada wa Ugogoni, Dada Chemi na wengine wengi. Tupashane habari na tuwapashe wengine.

1 comment:

Mjengwa said...

Kaka Banzi!
Wewe tayari umeshakuwa Mwanablog!
Karibu sana!
/maggid