Wednesday, December 13, 2006

EL SAEDY BUS MNABOA KINOMA!

Kwa wale waliopata bahati ya kusafiri kwenda Kilosa mkoani Morogoro si rahisi kulikwepa bus la EL-SAEDY.

Mwezi uliopita nilisafiri kwenda Ilonga Kilosa kuhudhuria harusi ya rafiki yangu Alphonce Kadeng'uka (Hongera sana KADE!). Baada ya kuanganisha mabus mawili hadi kufika Ilonga, bus la mwisho nilililopanda lilikuwa ni la El- SAEDY kubwa.

Nasema mnaboa kinoma, kwanza kondakta alinipa ticket ambayo haikuonyesha mmiliki wa Bus na namba ya gari. Lakini nilimezea tu mradi kufika.Hata nauli natumaini walinilangua, sawa tu. Lakini nilipoangalia karibu namlango nikakuta maandishi "SitAfu Kiti"(Ikiwa na maana ya Staff Seat) halafu amechanganya herufi kubwa na ndogo. Lakini mmiliki anaona ni sawa na abiria nao hivyo hivyo, traffic hivyo hivyo! Kweli mnaboa. Si ingeandikwa tu kwa kiswahili kuwa ni kiti cha mfanyakazi. Hata namba za viti zimeandikwa hovyo hovyo (kichefu chefu). Kumbukeni gari hilo limenunuliwa kwa mamilioni ya shilingi kwanini mnalichezea chezea hovyo. Rekebisheni haraka. Noma wazee

No comments: