Thursday, December 7, 2006

KUPASISHA MBEGU MPYA (SEED RELEASE)

Ndiyo, kuna mdau mmoja amekuja na hoja kuwa kwanini wataalamu wa kilimo huwa wanasema kuwa wametoa mbegu mpya lakini wakulima wanalalamika kuwa mbegu hizo hazipatikani. Mdau huyu alikuwa na maana ya "seed release" akitafsiri kwa kiswahili kuwa ni kutoa mbegu. Ukweli ni kwamba hapa mbegu inapasishwa tayari kwa matumizi kisheria.

Mchakato wa uzalishaji mbegu za mazao kwa kweli unatumia muda mwingi, utaalamu mbalimbali na nyenzo mbalimbali ambazo waliobobea huchukua miaka mingi kufuzu utaalamu huo na wakisha fuzu wanajulikana kuwa wataalamu wazalishaji vipando (plant breeders). Kabla mbegu haijatolewa kutumika, hufanyiwa tathmini na wataalamu, wakulima, wafanya biashara na walaji. Ikionekana inafaa ndiyo inapasishwa.

Ni tofauti kidogo na bidhaa kama vile vinywaji baridi- Kampuni ya Cocacola inapotoa aina mpya ya kinywaji wakati huo inakuwa tayari katika soko. Kwa mbegu za mazao si hivyo. Wanapopasisha mbegu ina maana kuwa mkulima anaweza kuitumia mbegu hiyo kiuzalishaji. Kabla haijapasishwa kama itatumika basi mtaalamu atakuwa hana makosa kama itagundulika kuwa ina hitilafu fulani. Hivyo ndivyo nilivyoelezwa na wataalamu wazalishaji vipando.

No comments: