Wednesday, December 13, 2006

BANGO LA PAROKIA YA MAKUBURI CHA MDORI!

Jumapili iliyopita nilitembelea eneo la "External" kule Mabibo sehemu inayojulikana kwa jina la Makuburi hapa jijini Dar Es Salaam. Kwa bahati nilipita karibu kabisa na Kanisa Katoliki la Makuburi(Enuerete Mwenye Heri- Mtanisahihisha wasomaji).

Kilichonishangaza, kwanza si rahisi kufahamu kuwa hilo ndilo Kanisa Katoliki la Makuburi kama nilivyoandika hapo juu. Kuna maandishi madogo sana ambayo ukipita kwa mbali hayawezi kusomeka halafu yameandikwa hovyo hovyo tu. Hayapendezi! Lakini karibu na maandishi hayo kuna maandishi makubwa kwenye ukuta yanayosomeka kuwa Computer Training Centre. Sasa nikajiuliza hapa shughuli kubwa ni training au kuabudu?

Waumini wa Makuburi, Katekesta, Paroko nawaulizeni hivi kweli mmeshindwa kuandika bango linaloonyesha Parokia yenu? Nafahamu Makuburi ni moja ya Parokia ambazo mnatoa sadaka kwa wingi siku za dominika, mavuno na michango mingine. Hivi Bango kwenu si muhimu? Aaa jamani andikeni bango jingine zuri lenye herufi za kusomeka. Tena msimike sehemu zile muhimu kama vile kwenye vituo vya "External" na "Garage" barabara ya Mandela na pale kanisani penyewe. Nafikiri mtafanya hivyo kabla ya Christmass. Nitapita tena, na kama bado nitaandika mbado!

No comments: