Wednesday, December 13, 2006

TICKETS ZA DALADALA TUNALIWA

Nafikiri wengi wetu tuishio hapa Dar usafiri wetu unategemea zaidi magari ya abiria yajulikanayo kama Daladala. Unaposafiri kwenye gari hilo unatakiwa upewe ticket inayoonyesha kiasi cha nauli kwa safari yako namba ya gari, mmiliki wa gari na tarehe ya kusafiri.

Wamiliki wa magari hayo wengi hutoa ticket hizo lakini cha kushangaza ticket hizo ni vipande vya karatasi vilivyokwishatumika kwa shughuli nyingine. Utakuta umepata ticket lakini nyuma inaonyesha mshahara wa mtu au mambo mengine kabisa ambayo hayana uhusiano na usafiri.

Hivi kweli wanaomiliki magari hayo wanafahamu maana ya ticket? Je, SUMTRA wanakagua ticket hizo? Ushauri wangu ni kwamba ticket zote za Daladala ziwe na "format" moja na kuwe na rangi tofauti kwa njia tofauti. Ikiwezekana ziwe na alama ya kuingia au kutoka kwenye kituo kilichopangiwa. Huu ndiyo ustaarabu au mpangilio mzuri. Ninakerwa sana nipolipa nauli yangu nakupewa karatasi isiyo namaana lakini naambiwa eti ni ticket!

No comments: