Monday, December 4, 2006

ELIMU NI KIOO?

Leo asubuhi nilikwenda Mkuranga (Makao Makuu ya Wilaya). Katika pita pita zangu nilisoma kibao kinachoonyesha kuwa mahali hapo ni Shule ya Msingi Mkuranga. Lakini kama ilivyo ada ya vibao vyote vya aina hiyo hapa nchini havikosi kauli mbiu. Kauli mbiu ya Shule ya Msingi Mkuranga ni " ELIMU NI KIOO." Nashindwa kupata tafsiri nzuri ya kauli mbiu hii. Je, Elimu ni kama kioo ambacho hutumika kukupa muono wa kitu fulani? Au Elimu ni kitu cha kutunza kwa uangalifu kwani kikikuponyoka ni vigumu kurudi katika hali yake (kioo kikivunjika). Je ni kweli? Wasomaji nisaidieni.Nimeshasoma kauli mbiu nyingi ambazo kwa kweli hazijitoshelezi. Nyingine zinakuwa ndefu mno na kukosa maana nyingine hazina uhusiano wowote na hali halisi. Tuwe makini katika kuandika kauli mbiu!

No comments: