Sunday, May 24, 2009

CETAWICO KUTATUA SOKO LA ZABIBU


Kiwanda cha mvinyo cha CETAWICO kilichopo Dodoma (Hombolo) kimedhamiria kuondoa tatizo la soko la zabibu kwa wakulima wa zao hilo. Hayo yalisemwa na Mhandisi Njovu alipoongea na Banzi wa Moro hivi karibuni alipotembelea kiwanda hicho katika shughuli za kupelemba na kutathmi shughuli za utafiti kanda ya kati. Uhakika huo unatokana na kiwanda hicho kupanua uwezo wa kuzalisha mvinyo kwa kuboresha mitambo na vifaa vingine. CETAWICO kwa sasa inazlisha aina kadhaa za mvinyo zikiwemo zile za Presidential na The Last Super.Bei ya zabibu kwa sasa ni kati ya Tshs 500-800 kwa kilo. Kwa muda mrefu wakulima wa zabibu wamekuwa wakilalamikia soko la zao hilo na kusababisha uzalishaji wa zabibu kushuka hapa nchini.

No comments: