Sunday, May 24, 2009

Hombolo waendelea na utafiti wa mtama

Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Hombolo iliyopo mkoani Dodoma kanda ya kati iko mbioni kutoa aina mpya za mtama zinazoweza kuhimili ukame na kuzaa kwa wingi pamoja na kutoa aina ya mtama itakayoweza kutumika kwa kutengeneza nishati (mafuta). Akiongea na blog hii hivi karibuni, Mtafiti Mkuu Bw. Letayo alisema kuwa tafiti hizi zinafanyika kwa ushirikiano na Asasi ya Utafiti ya Kimataifa ijulikanayo ICRISAT. Utafiti unaendelea vizuri na matokeo ya awali yanaonyesha mafanikio.

No comments: