Sunday, May 24, 2009

Mbuzi wa asili 'gogo white" kuboreshwa


Watafiti wa mifugo kutoka Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Nchini (NLRI) wameanza utafiti wa kuboresha mbuzi wa asili wajulikanao kwa jina la "gogo white" ili waweze kupata aina mpya ya mbuzi atakayeweza kuwa na sifa za kutoa nyama nyingi na nzuri pamoja na maziwa ya kutosha na pia kuhimili magonjwa na wadudu. Kazi hii ya utafiti tayari imeshaanza katika vituo cha Utafiti wa Mifugo Mpwapwa na Kituo cha Utafiti wa Malisho cha Kongwa vilivyopo Dodoma. Iwapo watafanikiwa basi wataweza kutoa jawabu kwa wafugaji wa mbuzi wanaopenda kufuga mbuzi aina ya "gogo white." Blog hii ilipata kuwaona mbuzi hao hivi karibuni wakiwa katika sehemu zao za utafiti. Mbuzi hao wanavutia kwa rangi zao nyeupe na maumbo yao.

No comments: