Tuesday, May 26, 2009

Wakulima wa alizeti waanza kuzalisha mbegu bora

Wilaya ya Iramba inatarajia kuboresha uzalishaji wa alizeti kutokana na mpango waliouanzisha kwa baadhi ya wakulima kuanza kuzalisha mbegu bora za alizeti.Hali hiyp imebainika baada ya watafiti wa kilimo na mifugo kutoka makao makuu ya Wizara ya Kilimo na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Mifugo kutembelea wilaya hiyo hivi karibuni kwa lengo la kupelemba na kutathmini shughuli za utafiti kanda ya kati.

Mbegu bora ya alizeti inayozalishwa inatarajiwa kuuzwa kati ya shilingi 2000 na 2500 kwa kilo na kupatikana kwa urahisi kwa wakulima huko vijijini. Aina ya mbegu ya alizeti inayozalishwa ni Record.

No comments: