Tuesday, May 26, 2009

Iramba ni alizeti

Leo nilisafiri kwenda wilaya ya Iramba kuona shughuli za kilimo zinavyoendeshwa na wakulima wa wilaya hiyo na hususan jinsi watafiti na wagani wanavyopeleka teknolojia kwa wakulima.

Lazima nikiri kwamba hii ni mara yangu ya kwanza kufika Iramba. Nikiwa njiani nilivutiwa na mashamba ya alizeti yaliyolimwa kando kando ya barabara ya kwenda Mwanza. Mashamba ni ya ukubwa wa wastani.Licha ya ukame ulioikumba kanda ya kati alizeti imekubali. Msafara wetu ulipata kufanya mazungumza na afisa wa kilimo wa wilaya na kueleza kuwa hali inavyoonekana uzalishaji mwaka huu utaongezeka ukilinganisha na mwaka wa jana na kwa hali hiyo kuna hatari ya kuwa na tatizo la soko la alizeti. Kwasasa gunia linauzwa kwa bei ya Tshs 15,000 wakati msimu wa mwaka jana gunia moja liliuzwa kwa bei ya Tshs 30,0000. Kweli Iramba ni alizeti.

No comments: