Tuesday, May 26, 2009

Si rahisi kwa mfugaji kutoa idadi ya mifugo yake

Ni masaa machache tangu niondoke kijiji cha Kaselya wilayani Iramba. Timu yetu ya Kupelemba na kutathmini ilifika hapa kuona jinsi ng'ombe aina ya Mpwapwa walionunuliwa na baadhi ya wafugaji katika kijiji hicho mwaka 2005 wanavyofugwa na kunufaisha wafugaji. Ng'ombe wanaendelea vizuri na lengo la kuboresha ng'ombe wa asili kwa kupitia madume ya Mpwapwa linaonyesha kufanikiwa. Jambo ambalo sikulitegemea ni kwa mfugaji mmoja kukataa kutoa idadi ya ng'ombe alionao.

No comments: