Sunday, May 24, 2009

Kichwa kikubwa cha alizeti

Nilipotembelea Taasisi ya Utafiti wa Kilimo ya Hombolo hivi karibuni nilivutiwa na mimea ya alizeti yenye vichwa vikubwa nikidhani kuwa kichwa kikubwa ni ubora wa alizeti lakini kumbe sivyo, watafiti walinieleza kuwa ili kuwa na mbegu nyingi za alizeti zilizojaa vizuri mmea unatakiwa kuwa na kichwa cha wastani. Ukitaka kufahamu zaidi kuhusu hilo wasiliana na watafiti wa mazao wa kituo cha Hombolo au kwenye vituo vya utafiti wa mazao vilivyopo karibu nawe. Kweli pua kubwa si wingi wa makamasi!

No comments: