Thursday, May 14, 2009

Unapochelewa "flight"

Usafiri wa ndege ni tofauti kabisa na usafiri wa bus. Kabla ndege haijapaa. Abiria hupitia mchakato unaochukua muda mrefu. Ndiyo maana unaambiwa ufike kiwanjani saa 2.00 au moja kabla ya safari kuanza. Kwani kuna ukaguzi wa ticket, pasi mizigo na usalama wa abiria. Unapofika kiwanjani dakika 45 kabla ya safari kuanza mara nyingi unahesabiwa kuwa umechelewa na kwa kweli ndege haiwezi kukusubiri. Usafiri wa bus ni tofauti kabisa hata ukichelewa unaweza ukakodi taxi ukalikimbiza bus na kupandia Kibaha! Lakini ndege utaikatizia wapi! Banzi wa Moro anawatahadharisha wanaosafiri kwa ndege kufika uwanjani mapema kupeleka usumbufu usio wa lazima unaoweza kusababisha kukosa safari au kubadilisha flight kwa kulipia gharama nyingine hivyo kufanya kuchelewa unakotakiwa kwenda na kuharibu mipango yote hasa unapokwenda kwa safari ya kikazi.

No comments: