Sunday, May 24, 2009

Tatizo la usafiri mikoa ya kati na ziwa sasa kuwa historia

Leo hii mchana nimewasili Singida mjini nikitokea Dodoma kikazi. Kilichonifurahisha ni kuona kuwa sehemu kubwa ya matengenezo ya barabara imekamilika. Mlima mbaya wa Saranda uliokuwa unawatesa madereva umeshatiwa lami. Ni sehemu ndogo kabisa ambayo bado haijakamilika. Njiani tulikutana na mabus kutoka Mwanza na Tabora yakifukia na ni mengi. Ndo maana nasema kuwa barabara hiyo itakapokamilika usafiri kwa mikoa ya kati na ziwa utaboreshwa kwa kiwango kikubwa na utakuwa ni wa uhakika zaidi.

No comments: