Tuesday, June 2, 2009

Omari Shomari-Dereva Mwandamizi


Omari Dogo ndivyo anavyojulikana dereva mwandamizi wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika. Omari ni dereva kijana lakini mwenye elimu ya kutosha na uzoefu wa muda mrefu katika uendeshaji wa Magari.


Dogo Omari anauzoefu wa zaidi ya miaka 15 ya uendeshaji gari katika ofisi za serikali. Mwaka wa jana alihitimu elimu ya Kidato cha Nne na umehudhiria kozi nyingi za muda mfupi hapa nchini.


Omari ameshasafiri karibu mikoa yote ya Tanzania Bara akiendesha magari madogo na makubwa. Ubora wa dereva Omari unatokana na jinsi anvyotunza gari, uendeshaji wa makini na kujali muda na vilevile ni mkweli katika kutenda kazi. Kijiko yeye atakiita kijiko na si umma.


Omari hujali familia ameoa na kubahatika watoto wawili wakike na kiume wanaosoma WhiteAngels English Medium Primary School - Kisemvule Vikindu Mkoa wa Pwani. Maskani yake ni Mbagala Charambe.

No comments: