Saturday, June 27, 2009

Wabunge mnawaumiza wafanyakazi wa serikali

BUNGE hili la bajeti limekuwa kali kweli kweli kila mmoja anaongea tena kwa jazba! Hakuna anayefuata sheria na taratibu. Lakini kibaya zaidi ni wabunge kuwafanya wafanyakazi wa serikali wasipumue huku wao wakipitisha maslahi yau bora zaidi kimya kimya. Huu ni unafiki.Eti oh mikutano na warsha stop! Huku wao wakiendesha mikutano. Serikali bila mikutano na warsha itaendeshaje shughuli zake. Chai na vitafunwa vimezidi, posho kwa kazi nzuri (Honorarium) ondoa. Sasa huyu mafanyakazi mnayemtaka afanye kazi kwa tija bila kumpatia mazingira mazuri ya kufanya kazi hiyo tija itapatikanaje? Ongezeni mishahara iwe ya kuvutia basi. Wabunge msikurupuke tu na hoja muwe makini vinginevyo sisi tunafikiri ni kujisafishia njia kwa uchaguzi wa mwakani.

No comments: